Mamlaka za DRC zatangaza visa 900 vinavyohusiana na Ebola

Mamlaka za nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimesema visa vinavyohisiwa kuwa vya Ebola vimeongezeka na kufikia 900, katikati ya mlipuko wa ugonjwa huo Mashariki mwa taifa hilo.

Hivyo taarifa ya Wizara ya Mawasiliano iliyochapishwa kwenye mtandao wa X jana Jumapili imesema kulikuwa na visa 904 na vifo 119 vinavyohisiwa vimetokana na maambukizi ya Ebola.

Hata hivyo mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya ulimwenguni WHO Tedros Adhanom Gebreyesus amethibitisha takwimu hizo na kuongeza kuwa juhudi za ufuatiliaji zinazidi kuimarishwa. 

Aidha mamlaka za Kongo hapo kabla zilitangaza zaidi ya visa 700 vya Ebola na zaidi ya vifo 170 vilivyoripotiwa zaidi kwenye jimbo la Ituri ambako ndio kitovu cha mlipuko huo.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii