Ujerumani iimesema itatoa euro milioni 20 zaidi kwa Sudan mwaka huu, huku ahadi zaidi za ufadhili zikipitiwa upya msaada huo unatolewa huku mzozo wa Sudan ukiingia mwaka wake wa nne Jumatano.
Ujerumani itatoa euro milioni
20 zaidi kwa Sudan mwaka huu, huku ahadi zaidi za
ufadhili zikipitiwa upya kwa sasa.
Hayo yamesemwa leo na wizara ya maendeleo ya Ujerumani mjini
Berlin katika taarifa, huku wafadhili wa kimataifa wakikusanyika kwa mkutano wa
tatu wa kimataifa kuhusu Sudan ikiwa imetimia miaka mitatu kamili tangu kuzuka
vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Mwishoni mwa mwaka wa 2025, wizara hiyo ilikuwa imetoa euro
milioni 155.4 kwa miradi nchini Sudan na katika nchi jirani zilizoathiriwa na
vita nchini Sudan, ambazo ingeongeza mwaka huu kwa euro milioni 20.
Kabla ya mkutano Berlin shirika la misaada la Save the Children
tawi la Ujerumani limetoa wito kufanyike juhudi kubwa zaidi za kuwalinda raia
Sudan.
Afisa Mkuu mtendaji wa shirika hilo Florian Westphal ametoa wito hatua zichukuliwe kukabiliana kikamilifu na mgogoro wa Sudan na kutaka mkutano wa Berlin ulete tija katika kuutafutua ufumbuzi mzozo huo.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime