Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema vita vya Iran vimesababisha mkwamo katika juhudi za kuvimaliza vita vinavyoendelea nchini mwake dhidi ya Urusi na hata kutatiza msaada wa silaha kutoka Marekani.
Zelensky ameliambia shirika la
utangazaji la Ujerumani, ZDF kwamba hivi sasa wapatanishi wa ngazi ya juu wa
Marekani "hawana muda kwa ajili ya mzozo wa Ukraine" na wamewekeza
nguvu katika kushughulikia vita vya Iran.
Amesema wajumbe wa Rais Donald Trump ambao ni Steve Witkoff na
Jared Kushner, waliokuwa na jukumu la kuratibu mazungumzo na Urusi ili
kuvimaliza vita vya Ukraine, hivi sasa wanaongoza majadiliano kati ya Marekani
na Iran.
Kwenye mahojiano hayo na ZDF, kiongozi huyo wa Ukraine, ameelezea wasiwasi kwamba iwapo Marekani haitoongeza shinikizo kwa Rais Vladimir Putin vita vinavyoendelea havitafikia mwisho.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime