SERIKALI imesema
imeweka mkakati wa kutangaza madini ya tanzanite nchini Qatar ili kuongeza wigo
wa masoko yake na kuvutia uwekezaji na utalii.
Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema hayo alipotembelea ofisi ya Ubalozi wa
Tanzania nchini Qatar na
kufanya mazungumzo na watumishi wa ubalozi. “Soko la tanzanite miaka ya hivi
karibuni lilionekana kushuka kidogo na ndiyo maana hata bei imeshuka.
Amesema mkakati huo wa
serikali ni muhimu na umekuja wakati mwafaka kwa kuwa baadhi ya nchi hazifahamu
kama madini ya tanzanite yanatoka Tanzania.
Hata hivyo amesema Tanzania imebarikiwa madini ya
aina mbalimbali yakiwamo ya vito lakini tanzanite ni ya kipekee na ni
utambulisho wa taifa hili kwa kuwa madini hayo hayapatikani popote duniani
zaidi ya Tanzania.
#10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime