Jeshi la Israel limewaua washukiwa wanne wanamgambo waliokuwa wamejihami na silaha walipojitokeza kutoka kwenye handaki katika eneo la Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza.
Jeshi la Israel limesema limewaua watu wanne wanaoshukiwa kuwa wanamgambo waliowashambulia vikosi vake wakati wanaume hao waliokuwa na silaha walipotoka kwenye handaki katika eneo la Rafah kusini mwa Gaza.
Jeshi limethibitisha katika taarifa yake kwamba magaidi wanne wenye silaha walitoka kwenye handaki la chini ya ardhi na kuwafyatulia risasi wanajeshi eneo la Rafah na baada ya kutambuliwa, wanajeshi wakawaangamiza magaidi hao.
Jeshi pia limesema hakuna mwanajeshi aliyejeruhiwa katika shambulizi hilo dhidi ya maafisa wake ambalo limelieleza kuwa ni ukiukaji wa makubaliano ya usitishaji mapigano katika Ukanda wa Gaza kati ya Israel na Hamas.
#10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime