RSF yatangaza kusitisha mapigano kwa miezi mitatu

Kundi la RSF limetangaza kusitisha mapigano kwa muda wa miezi mitatu hatia inayokuja ikiwa imepita siku moja baada Jeshi la sudan kukataa wito wa kimataifa wa kustisha vita unaongozwa na Marekani, kwa madai ya kuwepo kwa mapendeleo.

Kwenye hotuba iliyotolewa kupitia Televisheni  Kamanda wa RSF Mohamed Hamdan Dagalo alitangaza kuwa kwa pamoja kundi hilo lilikubaliana  kusitisha  vita kwa muda ili kuruhusu utoaji wa misaada na kulinda raia.

Hata hivyo Dagalo aliahidi kuzingatia  mfumo wa  majadilino unaoshirikisha  MisriSaudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu, na Marekani -- pamoja na Umoja wa Afrika na mashirika mengine ya kimataifa, ili kuhakikisha na kuruhusu misaada kuwafikia raia.

Tangazo hilo  la RSF limekuja baada ya mkuu wa jeshi la Sudan Abdel Fattah Al-Burhan kukataa pendekezo hilo la kusItisha vita kwa misingi ya mapendeleo kwa kundi la RSF. 

RSF imeshutumiwa na makundi ya kutetea haki za binadamu na wanadiplomasia kwa kutekeleza  ukatili mkubwa  , ikiwa ni pamoja na mauaji ya zaidi ya raia 2,000 huko El Fasher, jiji kuu la Darfur ambalo kundi hilo liliuteka kutoka kwa jeshi mwezi Oktoba.

Mapigano kati ya jeshi na kundi la  RSF yalizuka mwezi Aprili 2023 na yameua maelfu na mamilioni ya watu kuyahama makazi yao, na vita hivyo kuwa  moja wapo ya migogoro mbaya zaidi ya kibinadamu kuwahi kuripotiwa duniani.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii