Dkt. Mwinyi" Nitaendelea Kuimarisha Udhamini Na Miundombinu Ya Michezo"

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaendelea kufanya kila juhudi kuhakikisha wadhamini katika sekta ya michezo wanapatikana, ili kukuza vipaji na kuinua ustawi wa michezo nchini.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 26 Oktoba 2025, baada ya kuongoza matembezi ya wanamichezo kutoka vikundi vya mazoezi ya viungo, vilivyoanzia Hoteli ya Bwawani, kupitia Darajani–Michenzani hadi Viwanja vya Michezo vya Maisara, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Amesema kuwa upatikanaji wa wadhamini utasaidia kukuza vipaji vya vijana, jambo litakaloiwezesha Zanzibar kupata wanamichezo bora watakaoiwakilisha nchi ndani na nje ya mipaka yake.

Dkt.Mwinyi amesema Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi na wadau mbalimbali kuhakikisha michezo inapata udhamini wa kutosha, ili kukuza vipaji na kutoa ajira kwa vijana wetu.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii