Mpinzani wa Museveni Besigye amegoma kuhudhuria kesi

Mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda, Kizza Besigye, amegoma kuhudhuria kesi yake ya uhaini akimtuhumu jaji anayesimamia kesi hiyo kuwa na upendeleo.

Besigye, aliyewahi kuwa daktari wa Rais Yoweri Museveni na mgombea wa nafasi ya urais mara nne nchini Uganda, anashikiliwa na mamlaka za kiusalama kwa tuhuma za uhaini dhidi ya serikali.

Ifahamike kuwa Besigye aliwekwa kizuizini pamoja na msaidizi wake Novemba 2024 katika nchi jirani ya Kenya na kurejea Uganda, ambapo wote wawili walishtakiwa kwa uhaini na makosa mengine awali katika Mahakama ya Kijeshi kabla ya kesi hiyo kuhamishiwa katika Mahakama ya Kiraia.

Imeelezwa kuwa Besigye alitakiwa kufika mahakamani jana Jumatatu kusikiliza kesi yake, iliyocheleweshwa kwa miezi kadhaa, lakini aligoma akimtaka jaji anayesimamia kesi hiyo, Emanuele Bugumu, kujiondoa.

Taarifa iliyotolewa na wakili wa Besigye, Eron Kiiza, imesema kuwa kiongozi huyo ameamua kususia kesi yake mpaka pale Mahakama itakapowasikiliza na kufanya uamuzi wa kumuondoa wakili anayesimamia kesi hiyo kwa sasa.


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii