Mtoto wa Waziri mkuu wa Mongolia ajiuzulu sababu ya kuendekeza Starehe kazini

Waziri Mkuu wa Mongolia, Oyun-Erdene, amejiuzulu kufuatia maandamano makubwa yaliyozuka baada ya mtindo wa maisha ya kifahari wa mwanawe kuonekana kwenye mitandao ya kijamii.

Mwanawe ameonesha mifuko kadhaa yenye manunuzi alipokuwa kwenye likizo ya uchumba ambapo imeonesha ni matumizi ya gharama kubwa.

Wakiwa kwenye likizo hiyo, inaripotiwa mchumba wake alipost mtandaoni picha iliyokuwa na maelezo yaliyosomeka: “Happy birthday to me” (Heri ya siku yangu ya kuzaliwa). Picha nyingine ilionyesha wanandoa hao wakibusiana wakiwa katika swimming pool.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii