MBUNGE ANYWA BIA KWENYE KIATU BUNGENI

Mbunge wa Chama cha Wafanyakazi Australia Magharibi Kyle McGinn amemaliza muda wake wa mihula miwili Bungeni kwa kuvua kiatu chake na kumimina bia kwenye kiatu na kisha kunywa.

McGinn amefanya tukio hilo wakati akitoa hotuba yake ya mwisho ambapo amesema kitendo hicho cha kunywa bia kwenye kiatu chake ni kitendo ambacho amekuwa akikifanya pamoja na wapiga kura wake na amefanya hivyo ili kuwashukuru wapiga kura wake waliomwamini kwa mihula miwili bungeni.

Nilifikiria kwa muda mrefu na kwa bidii kuhusu jinsi ningemaliza hotuba hii na wapiga kura wangu katika Goldfields nadhani watakuwa wa kushukuru sana kuna njia moja tu ya kuifanya na nimezoea kuambiwa, kwa hivyo tunaweza kumaliza lakini, ningependa kuwaambia wanachama na wapiga kura wote wa Chama cha Wafanyakazi, asante kwa kuniamini kwa mihula mawili mizuri cheers.” Alisema mbunge Kyle McGinn.

Aidha McGinn ameviambia vyombo vya habari nchini Australia kuwa alifanya hivyo ili kuonyesha kulikuwa na watu wa kawaida bungeni na kusherehekea kwa njia yake mwenyewe.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii