Kwanini binadamu hufurahia kula kwa pamoja?

Kwa miongo sasa, wanadamu wamekuwa wakikusanyika kwa vikundi vidogo kula chakula pamoja. Kwa nini ni muhimu – na kwa nini tunaendelea na mila hii?

Kula chakula pamoja ni jambo la kawaida sana kwa wanadamu. Mikusanyiko ya chakula na marafiki, sherehe za chakula, na mikusanyiko ya likizo ambapo mara nyingi tunajizidisha – kula chakula pamoja ni jambo linalofanyika kila siku, kiasi kwamba mara nyingi halizingatiwi isipokuwa pale ambapo watu wanahisi kuwa halitendeki vya kutosha, jambo ambalo linaweza kuwa na umaarufu kwa wakati mwingine.

Ni hofu kubwa kuhusu kupungua kwa mikusanyiko ya familia kwa chakula, kwa mfano, mara nyingi hugonga vichwa vya habari.Kula pamoja, inaonekana, si jambo la kawaida tu, bali ni jambo lenye nguvu kubwa. Lakini kwa nini?

Kula chakula kwa pamoja inaweza ikaturudisha nyuma enzi zile za asili ya spishi yetu. Sokwe na bonobo, ndugu zetu wa karibu zaidi mamalia wa hali ya juu pia hula kwa pamoja na makundi yao ya kijamii.

Hata hivyo, kusaidia watu na chakula si sawa na kula pamoja, anasema mwana-sosholojia Nicklas Neuman kutoka Chuo Kikuu cha Uppsala, Sweden. “Unaweza kugawa chakula kama bidhaa bila kukaa chini na kula na wengine,” anasema. Wanadamu wanaonekana wameongeza na kujenga desturi kwenye shughuli hii ya kula kwa pamoja.

Ingawa hakuna anayejua kwa hakika ni lini wanadamu au mababu zetu walijifunza kupika, ikakadiriwa ilianza miaka milioni 1.8.

Hata hivyo, wakati mtu anapojitahidi kuwinda au kukusanya chakula, kuwasha moto, na kupika, inaonyesha kuwa alikuwa na kundi la kijamii kumsaidia katika hatua zote za maandalizi ya kupika chakula.

 

Pindi mnapokaa karibu na Moto ,huku giza likitanda ,utagundua kuwa unapendelea kukaa muda mrefu zaidi.

Robin Dunbar, mtaalamu wa antropolojia kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, anaamini kuwa masaa hayo ya ziada yanaweza kuwa fursa muhimu ya kuimarisha uhusiano wa kijamii kwa kula pamoja.

Utafiti wa Dunbar ulionyesha kuwa kula chakula na wengine mara kwa mara kunahusiana na kuridhika zaidi maishani na kuwa na marafiki wa kutegemea msaada.

Utafiti huo ulionyesha kuwa mikusanyiko ya chakula ni chanzo cha athari za kijamii, na si matokeo ya hizo athari.

“Kula chakula huamsha mfumo wa endorfinu wa ubongo, ambao unaoana kati ya wanadamu na mamalia wa hali ya juu,” anasema Dunbar.

“Kula pamoja kama kundi kunaimarisha athari hii ya endorfinu kwa njia ile ile kama vile kufanya mazoezi pamoja. Hii inatokea kwa sababu shughuli zinazofanyika kwa wakati mmoja huongeza uzalishaji wa endorfinu maradufu.”

Kula chakula kilekile kwa wakati mmoja na mtu mwingine hufanya mtu huyo kuwa na uaminifu zaidi. Utafiti uliofanywa na waandishi wa habari Cynthia Graeber na Nicola Twiley katika podcast yao Gastropod ulionyesha kuwa katika mfano wa uwekezaji, watu walitoa fedha zaidi kwa mtu waliyekula pipi sawa na yeye hapo awali.

Vile vile, watu waliokula vibanzi sawa walikuwa haraka kuafikiana kwa mazungumzo kuliko wale waliokula vibanzi tofauti.

Ayelet Fishbach kutoka Shule ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Chicago aligundua kuwa ladha zinazofanana katika chakula zinaweza kuwa ishara ya maadili yanayoshirikiana, ingawa hii ni jambo linaloweza kutofautiana kwa wakati wa sasa.

Hata hivyo, kula pamoja si kitendo kilicho na athari chanya kila mara. Sherehe za chakula, ambapo chakula kingi kinashirikishwa, zinaweza kuwa njia za kuonyesha mamlaka au udhibiti.

Hebu fikiria desturi ya mavuno abapo mkulima hutoa mlo mwimgi kwa wafanyakazi wake, au sherehe ya ofisini ambapo ukarimu wa mwajiri, au ukosefu wake, unachunguzwa na waliohudhuria.

Mikusanyiko ya chakula ya familia, ingawa inasifiwa, si lazima iwe bila migogoro.

 

“Watu wanasema wanapenda kula chakula na marafiki na wapendwa. Lakini inaweza pia kuwa ni uzoefu mbaya kula pamoja na wapendwa,” anasema Neuman. “Ni mahali pa kudhibiti na kutawala pia.”

Kula kwa pamoja ambapo mtu anakosoa uamuzi wako au uzito wa mwili wako ni eneo ambalo halikusaidii maishani.

Katika utafiti mwingine unaohusu mtazamo wa wazee nchini Sweden, Neuman aligundua jambo la kushangaza.



“Tuliwauliza kwa makusudi kama wanahisi kudhuriwa na kula peke yao. Wengi wao hawaoni shida,” anasema. Wanapenda kula na wenzao, lakini wengi wao hawahisi upungufu wa hilo kama vile ungetarajia. Pengine hili linahusiana na hali ya upweke, anadhania: kama mtu anajihisi upweke, basi kula peke yake huenda kukaongeza usumbufu.

“Lakini kama wewe ni mtu ambaye mara kwa mara unakula na wengine, basi pengine, wakati mwingine,” anasema Neuman, “itakuwa vizuri kukaa peke yako na kusoma kitabu.”

 

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii