Waganga wakataa kuhusishwa na matukio ya ukatili

Waganga wa Tiba asili waomba kutohusishwa na matukio ya ukatili yanayotokea kwenye jamii kwani wao hawahusiki na kuwatuma watu wafanye ukatili badala yake wameomba kupewa thamani kama ambavyo madaktari wa Hospitalini.

Waganga wamesema wanataka kuthaminiwa kama madaktari wa hospitali, kwani dawa zote za hospitali zilitokana na dawa za asili zikaboreshwa ndio zikatumika Hospitali.

Wamesema vitendo vingi wamekuwa wakitajwa lakini sio kweli kama wanatumika isipokuwa watu wamekosa utu ndio maana wanatekeleza matukio hayo.


Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii