Awamu ya kitaifa ya mashauriano kuhusu mustakabali wa vyama vya siasa yafunguliwa

Nchini Mali, awamu ya kitaifa ya mashauriano ya "vyama vya siasa" nchini humo kuhusu mapitio ya Mkataba wa Vyama vya Kisiasa vya Mali imefunguliwa siku ya Jumatatu, Aprili 28, 2025 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Bamako (CICB) huko Bamako. Shughuli hizo ambazo zinahitimisha kazi iliyoanzishwa Aprili 16 na 17 katika ngazi ya mkoa, itaendelea hadi kesho Jumanne.

Uhalali wa kijadi au kidini, haswa, pamoja na Wamali waishio nje ya nchi, wanaalikwa kutoa mapendekezo ya kupunguza idadi ya vyama vya kisiasa na kudhibiti ufadhili wao. Lakini kwa wiki kadhaa wanasiasa wamekuwa wakilaani mbinu iliyokusudiwa kuwafanya kutoweka.

Nchini Mali, mamlaka ya mpito haijachapisha nyaraka rasmi kuhusu kufanyika kwa mashauriano haya, kwa mfano juu ya mbinu za kuchagua wawakilishi wa "vyama vya siasa" vilivyoalikwa kutoa mapendekezo yao. Vyanzo mbalimbali vya serikali vilivyowasiliana na RFI havikuweza kutoa maelezo yoyote.

Kuvujwa kwa vyama vya siasa

Mnamo Aprili 16 na 17, 2025, mashauriano ya kimkoa tayari yalitoa pendekezo muhimu: uvunjaji safi na rahisi wa vyama vyote na kuunda vyama vipya viwili au vitatu kuchukwa nafasi ya vyama hivyo vinavyokuwa vimevunjwa.

Ni nini hasa vyama mia moja vilivyoungana ndani ya Mpango wa Vyama vya Siasa kwa Mkataba (IPAC) viliogopa na kutangaza, hata kabla ya mashauriano kuanza.

IPAC, ambayo inaleta pamoja vyama vyote vya kihistoria na uwakilishi nchini, yenyewe ilikuwa imewasilisha mapendekezo yake mwezi uliopita ili kupunguza wingi wa vyama vilivyopo, na kudhibiti na kuweka masharti ya ufadhili wao wa umma ili kukomesha dhuluma.

Mwisho wa mfumo wa vyama vingi?

Malengo ya pamoja, kwa hivyo, kwa mamlaka ya mpito, vyama vya kisiasa na Wamali wote ambao walikuwa wametoa, haswa wakati wa Mkutano wa Kitaifa wa Urekebishaji. Bila kutaja kufutwa.

Leo, wanasiasa, pamoja na watetezi wote wa mafanikio ya kidemokrasia ya mwaka 1991 - mwaka wa kuanguka kwa udikteta wa kijeshi wa Jenerali Moussa Traoré - wanaabaini kwamba mashauriano haya yanayotafutwa na mamlaka ya mpito yanaficha nia iliyofichwa vibaya ya kukomesha mfumo wa vyama vingi, ambao hata hivyo unahakikishwa na Katiba ya Mali, kwa uhalali wa uwongo. Kazi hiyo inatarajiwa kukamilika kesho.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii