Wanaolazimisha ununuzi Sare, Daftari katika shule zao kukiona

Serikali imesema itawadhibu vikali Walimu wakuu walio na tabia na ambao wataendelea kuwalazimisha wazazi kununua sare za wanafunzi kutoka kwenye maduka fulani au ndani ya shule zao zinazouza vifaa ghali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Katibu katika Wizara ya Elimu nchini Kenya, Belio Kipsang imeeleza kuwa mwenendo huo uliotolewa malalamiko na wazazi ni kinyume cha Sheria ya Elimu ya Kimsingi na kanuni kuhusu Elimu ya Msingi 2015.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii