Waombolezaji nchini Iran wameendelea kujitokeza kwa wingi mjini Tehran kwa siku ya pili mfululizo katika kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Kiongozi wa juu zaidi nchini humo, Ayatollah Ali Khamenei.
Ibada maalumu ya kumuombea Khamenei aliyeuwawa katika mashambulizi ya Israel na Marekani mwezi Februari, imefanyika katika Msikikiti wa Grand Mosalla na kuongozwa na mwanazuoni mashuhuri wa Kiislamu wa madhehebu ya Shia, Ja'far Sobhani.
Viongozi waandamizi wa serikali wahudhuria
Rais wa Iran Masoud Pezeshkian pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Iran akiwemo spika wa bunge Mohammad Bagher Ghalibaf, wamehudhuria ibada hiyo.
Iran imetangaza Jumapili kuwa siku ya mapumziko ya kitaifa. Zaidi ya watu milioni 10 wanatazamiwa kushiriki shughuli za kutoa heshima za mwisho. Mwili wa Khamenei utapelekwa Iraq na hatimaye unatarajiwa kuzikwa Alhamisi katika mji wa Mashhad alikozaliwa.
10YrsJembefm #Familiamoja #AhsantekwaTime