Viongozi wa Ulaya waunga mkono mazungumzo ya Ukraine, Urusi

Viongozi wa Uingereza, Ujerumani na Ufaransa wanaunga mkono pendekezo la mazungumzo kati ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy na Rais wa Urusi Vladimir Putin ili kujaribu kufikia makubaliano ya usitishaji mapigano.

Viongozi wa Uingereza, Ujerumani na Ufaransa wamesema wanaunga mkono pendekezo la mazungumzo kati ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy na Rais wa Urusi Vladimir Putin ili kujaribu kufikia makubaliano ya usitishaji mapigano.

 Katika taarifa ya pamoja, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer, Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron walipongeza wito wa Zelenskiy wa kukomesha vita na pendekezo lake la kuwepo mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Ukraine na Urusi, huku Marekani na Ulaya zikishirikishwa kikamilifu. 

Viongozi hao watatu, wanaoongoza muungano usio rasmi wa usalama unaoitwa E3 ambao ni mojawapo ya vyanzo vikuu vya msaada wa kimataifa kwa Ukraine, walijiunga na Zelenskiy Jumapili jijini London.

 Zelensky alimuandikia barua ya wazi Putin akipendekeza mkutano wa ana kwa ana lakini Rais huyo wa Urusi alikataa wazo hilo, akisema "hakuna maana" kukutana na Zelensky hadi makubaliano ya amani yatakapofikiwa.

Wakati huo huo, shambulio la droni za Ukraine dhidi ya treni ya abiria liliua mmoja wa madereva wake na kumjeruhi mwingine. Shambulio hilo lilitokea saa chache baada ya Urusi kufanya wimbi la mashambulizi ya droni na makombora mengine huko Ukraine, huku moja ya mashambulizi hayo yakiharibu kituo cha kuhifadhia silaha za nyuklia karibu na eneo la Chernobyl.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii