“Nimeamua kujiunga na CCM kwa sababu nimeona dhamira ya kweli ya serikali ya Dk. Samia katika kulinda amani na kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli. Amani ndiyo msingi wa maendeleo, na siwezi kuunga mkono harakati za kuvuruga hali hiyo,” alisema Wenje.
Wenje aliongeza kuwa amevutiwa na utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kama vile ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), maboresho ya miundombinu ya barabara, huduma za afya, elimu, na upatikanaji wa maji safi vijijini.
“Serikali hii inafanya kazi kubwa, miradi inaonekana kila kona. Nimeona ni heri niwe sehemu ya wale wanaounga mkono juhudi hizi badala ya kupinga kila kitu,” aliongeza.
“Sijaja hapa kwa chuki, nimekuja kwa sababu ya imani yangu kwa mustakabali wa taifa. Lakini napenda kusema wazi si kweli kwamba CHADEMA imezuiliwa kushiriki uchaguzi. Hizo ni propaganda,” alisema.