Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Magazeti ya Uingereza ya The Independent na The Guardian, Marehemu Martyn Latchman alikuwa akijiandaa kufanyiwa upasuaji wake wa pili katika kliniki hiyo baada ya upasuaji wake wa kwanza kufanikiwa ambapo hata hivyo kabla ya kuanza kwa mchakato wa pili, alizidiwa ghafla kwa sababu ambazo bado hazijafahamika.
Taarifa ya kliniki hiyo imesema kuwa Latchman aligundulika kuwa Mgonjwa kwa ghafla wakati wa maandalizi kabla ya upasuaji wa pili kuanza ambapo aliwaishwa katika chumba cha Wagonjwa mahututi katika hospitali ya karibu lakini alifariki dunia baadaye.
Mwili wa marehemu Latchman ambaye alihudumu kama Mwalimu Mkuu kwa zaidi ya miaka 16 huko Bedford kabla ya kubadili taaluma na kuwa Mkandarasi wa masuala ya Ulinzi, umerejeshwa Uingereza kwa uchunguzi zaidi huku Mamlaka za afya Nchini Uturuki zikianzisha uchunguzi wa kina ambapo nyaraka zote za matibabu zinazohusiana na tukio hilo zimewasilishwa kwa Mamlaka husika.
Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii