• Jumatatu , Aprili 28 , 2025

Wakazi 576,000 wa Gaza wako katika hatari ya kukabiliwa na njaa-UN

Takriban watu 576,000 katika Ukanda wa Gaza, robo ya wakazi wa Gaza wako katika hatari kubwa ya kukabiliwa na njaa, afisa mkuu wa Umoja wa mataifa aliliambia Baraza la usalama la Umoja wa mataifa Jumanne, akionya kwamba janga kubwa la njaa halitaepukika ikiwa hatua hazitachukuliwa.

“Kuna uwezekano mkubwa ikiwa mapigano yataendelea na kuna hatari yataibuka katika maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu kusini mwa Gaza. Kwa hivyo tunasisitiza wito wetu wa kusitisha mapigano, “ alisema Ramesh Rajasingham, mkurugenzi wa Ofisi ya Umoja wa mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu.

Mtoto mmoja kati ya watoto sita walio na umri wa chini ya miaka miwili kaskazini mwa Gaza anakabiliwa na utapiamlo mkali na kupoteza uzito wa mwili, na takriban watu wote milioni 2.3 katika eneo la Palestina wanategemea chakula kisichotosha ili kuishi, aliliambia Baraza la usalama la Umoja wa mataifa.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii