MAJARIBIO MTAMBO NO. 9 BWAWA LA NYERERE WAFANIKIWA

Mtambo wa kwanza wa kuzalisha umeme katika Bwawa la Mwalimu Nyerere umefanikiwa kuwashwa kwa majaribio hali itakayoboresha upatikanaji wa umeme nchini.


Hayo yamebainishwa na leo Februari 16 Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga wakati akijibu swali la Mbunge wa Luepmbe, Edwin Swalle aliyetaka kujua lini Mitambo katika Bwawa hilo itaanza kuwashwa.


“Mwezi wa 6 mwaka huu ndio tulikuwa tumepanga kuwasha Mtambo Namba 9 kwa mara ya kwanza. Lakini kwa jitihada za Serikali na Mkandarasi tuliweza kusogeza ratiba za kuwasha mtambo Namba 9 mpaka mwezi huu wa Pili.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii