DAVID JAY KUITEKA AFRIKA KIMUZIKI

David Jatta maarufu kwa jina la Sanaa David jay ni Mwimbaji & Mtunzi wa Nyimbo

Mwenye asili ya Denmark na Gambia. Alikulia katika utamaduni ambapo muziki na taswira ilikuwa kubwa  Alizaliwa na kukulia huko Copenhagen.

Kama msanii wa soul/RnB, David Jay alibadilika sana katika miaka michache iliyopita na anakua kwa kasi kama mwimbaji na mtunzi wa nyimbo. Upendo wake na mapenzi yake katika muziki vimemsaidia kutengeneza kiwango bora cha muziki na sauti thabiti ambayo imeweza kuvutia hadhira kubwa sana kimataifa .


Ikiwa muziki wa amapiano umekuwa na nguvu kubwa kwa sasa katika taswira ya muziki David jay pamoja na falva one wameamua kushirikiana Pamoja na kufanya kazi ya Pamoja ikiwa ni remix ya wimbo uitwao “bouncy”.

Wimbo huu pia ni moja kati ya kazi yake ambayo itafungua milango ya kazi zingine ambazo zinatazamiwa kutoka ndani yam waka 2023.

Vile vile unapatikana katika mitandao yote ya kijamii 

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii