Yaliyojiri Mahakamani Kesi ya Sabaya

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha leo Jumatano Desemba 29, 2021 imeshindwa kutoa uamuzi mdogo katika kesi inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake sita baada ya mawakili wa utetezi kushindwa kufika mahakamani.

 

Katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 27 ya mwaka huu, mbali na Sabaya watuhumiwa wengine ni Enock Mnkeni, Watson Mwahomange, John Aweyo, Sylvester Nyegu, Jackson Macha na Nathan Msuya.

 

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Patricia Kisinda upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Felix Kwetukia na Mwendesha Mashitaka wa Takukuru, Jacob Piyo.

 

Wakili Kwetukia alieleza mahakama kuwa upande wa watuhumiwa hakuna wakili hata mmoja na watuhumiwa wote wapo mbele ya mahakama hiyo.

 

“Leo upande wa watuhumiwa hakuna wakili hata mmoja ila watuhumiwa wote wapo. Shauri lilikuja kwa ajili ya uamuzi mdogo na kwa kuwa watuhumiwa wana uwakilishi wa mawakili ambao kwa siku ya leo hawapo,”alisema na kuongeza.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii