Watu 20 wauawa katika mashambulio la wanamgambo wa kijihadi Mali

Karibu watu 20 wameuawa katika shambulio linaotuhumiwa kutekelezwa na wapiganaji wa kijihadi kaskazini mwa Mali, ofisi ya kikanda katika eneo hilo inasema.

Ghasia za Jumamosi zilitokea karibu na mji wa Gao.

Afisa huyo aliambia shirika la habari la Ufaransa kwamba hali ilikuwa tete kwani raia walikuwa wakitoroka wakato wanamgambo hao walipokuwa wakifanya unyama dhidi yao.

Umoja wa Mataifa unasema hali ya usalama katika maeneo ya Gao na Ménaka imezorota vibaya.

Mapema Jumapili walinda amani wa Umoja wa Mataifa waliuawa karibu na mgodi mmoja huko Kidal kaskazini mwa nchi.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii