MSIMAMIZI wa tanki Kassim Kongwa na wenzake, wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa shataka la wizi wa lita 2,800 za mafuta ya ghafi mali ya kampuni ya Mikoani Edible Oil and Detergents Limited.
Washtakiwa wengine ni Hemed Abdallah, Hassan Kimoge, Juma Issah, Halfan Halfan maarufu kama Ruba, Maria Gulaba ambao ni opereta wa kiwanda hicho na mlinzi Jafar Molel.
Washtakiwa hao wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam na kusomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Anna Magutu.
Akiwasomea mashtaka, wakili wa serikali Winiwa Kasala alidai, kati ya Juni 2 na 4, mwaka huu jijini Dar es Salaam,kwa nia ovu, washtakiwa hao waliongoza genge la uharifu na kuiba mafuta ghafi mali ya kampuni hiyo.
Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii