Argentina yahaha kubaini chanzo cha virusi vya hanta

Mlipuko wa virusi vya hanta kwenye meli ya kitalii wazua taharuki huko nchini Argentina huku ikichunguzwa kama chanzo huku abiria wakipelekwa Ulaya kwa matibabu ya dharura.

Maafisa wa afya na wataalamu nchini Argentina wanahangaika kubaini iwapo nchi hiyo ndiyo chanzo cha mlipuko hatari wa virusi vya hanta ulioikumba meli ya kitalii katika Bahari ya Atlantiki.

Dharura hiyo ya kiafya imeibuka wakati Argentina ikishuhudia ongezeko la maambukizi ya virusi hivyo ambalo watafiti wa afya wanalihusisha na athari zinazoongezeka za mabadiliko ya tabianchi.

Argentina ambako safari ya meli hiyo kuelekea Antaktika ilianzia imetajwa mara kwa mara na Shirika la Afya Duniani kuwa miongoni mwa nchi zenye kiwango kikubwa zaidi cha maambukizi ya ugonjwa huo unaosambazwa na panya katika kanda ya Amerika ya Kusini.

Aidha abiria wapatao 40 kutoka meli hiyo tayari wameshuka katika kisiwa cha St. Helena Kusini mwa Bahari ya Atlantiki akiwemo mke wa raia wa Uholanzi aliyefariki kutokana na mlipuko huo.

Hata hivyo wakati huo huo ndege ya dharura iliyombeba mmoja wa wagonjwa kutoka meli hiyo imewasili Amsterdam nchini Uholanzi huku wagonjwa wengine wawili wakipelekwa Uholanzi na Ujerumani kwa matibabu zaidi.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii