Waziri Mkuu wa Uingereza afunguka mazito vita ya Iran na Marekani

Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, amesema amechoshwa na athari za kiuchumi zinazotokana na maamuzi ya Rais wa Marekani, Donald Trump, huku mvutano kati ya Ulaya na Marekani ukiongezeka kufuatia vita ya Iran.

Akizungumza katika mahojiano, Starmer alisema familia na wafanyabiashara nchini Uingereza wanaathirika na kupanda na kushuka kwa gharama za nishati, hali inayochangiwa na migogoro ya kimataifa.

“Nimechoshwa na hali ya kuona familia zikiteseka kutokana na mabadiliko ya bei za nishati yanayosababishwa na matukio ya kimataifa,” alisema Starmer.

Starmer alisisitiza kuwa suluhisho la kudumu ni kupunguza mvutano na kutumia diplomasia, akitaka kufunguliwa haraka kwa Strait of Hormuz, njia muhimu ya usafirishaji wa mafuta duniani.

Kauli hiyo imekuja wakati viongozi kadhaa wa Ulaya wakianza kuonyesha wazi kutoridhishwa na msimamo mkali wa Marekani katika mgogoro huo.

Vita ya Iran imeanza kuathiri kile kinachojulikana kama “uhusiano maalum” kati ya Marekani na Uingereza, huku Starmer akichagua msimamo wa tahadhari badala ya kujiingiza moja kwa moja kwenye vita.


Hatua hiyo imeibua ukosoaji kutoka kwa Trump, ambaye amewahi kumkosoa hadharani Starmer kwa kusuasua kushirikiana na Marekani katika operesheni za kijeshi.

Mbali na Uingereza, viongozi wengine wa Ulaya pia wameanza kujitenga na msimamo wa Marekani:

  • Pedro Sánchez alikataa kuruhusu Marekani kutumia vituo vya kijeshi vya Hispania
  • Emmanuel Macron alimtaka Trump kuwa makini zaidi katika kauli zake kuhusu vita
  • Kaja Kallas alieleza sitisho la mapigano kama “hatua ya kuondoka kwenye hatari kubwa”

Hatua hizi zinaonyesha mgawanyiko unaoongezeka kati ya washirika wa muda mrefu wa Magharibi.

10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii