Wakili poul muite"Rigathi Gachagua Amelazwa Karen Hospital Akiwa na Maumivu Makali ya kifua"

Oktoba 17, Wakili Mkuu Paul Muite alifichua kuwa alifanikiwa kuzungumza na madaktari wanaomhudumia naibu rais. 


Kulingana na Muite, kwa sasa Gachagua amelazwa The Karen Hospital baada ya kupatwa na maumivu makali ya kifua. Wakili huyo mkuu alifichua kwamba madaktari wa Gachagua walikuwa wamemshauri (Gachagua) kupumzika kabisa kwa muda. 


"Ningependa kuwafahamisha Waheshimiwa Maseneta kwamba nimeweza kuwasiliana na madaktari wa Hospitali ya Karen, na kwa sababu ya hali yake sikuweza kuzungumza naye moja kwa moja kwa ushauri wa madaktari wake ambao walisema lazima apumzike kikamilifu. wakati huo, hata hivyo, nilifahamishwa na madaktari wake kwamba kwa sasa anaugua maumivu makali ya kifua sikutaka kuuliza zaidi ya hapo.


Muite alimsihi Spika Amason Kingi kusitisha shughuli za kuondolewa kwake hadi tarehe iliyotangulia. 



Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii