Rosalynn Carter, mke wa Jimmy Carter amefariki akiwa na umri wa miaka 96

Rosalynn alikuwa mshirika wangu wa karibu katika kila kitu nilichowahi kukifanya, Rais wa zamani Jimmy Carter alisema katika taarifa iliyotolewa na Kituo cha Carter.

Mke wa rais wa zamani Rosalynn Carter, mwanaharakati wa afya ya akili, alifariki dunia akiwa na miaka 96 siku ya Jumapili akiwa nyumbani kwake huko Plains, kwenye jimbo la Georgia, Kituo cha Carter kimesema katika taarifa.

Rais wa zamani Jimmy Carter, mwenye miaka 99, na Rosalynn Carter walikuwa katika ndoa kwa miaka 77. Rosalynn Carter ameacha watoto ambao ni Jack, Chip, Jeff na Amy. Wajukuu 11 na vitukuu 14.

Rosalynn alikuwa mshirika wangu wa karibu katika kila kitu nilichowahi kukifanya, Rais wa zamani Jimmy Carter alisema katika taarifa iliyotolewa na Kituo cha Carter. Alinipa mwongozo wa busara na kunitia moyo wakati nilipohitaji. Kwa muda wote ambao Rosalynn alikuwa duniani, siku zote nilijua ni mtu aliyenipenda na kuniunga mkono.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii