FAIDA ZA KUTUMIA PUA KATIKA UPUMUAJI KULIKO MDOMO.

Kupumua ni mchakato muhimu sana ambao hauitaji kujifunza: sote tunapumua tangu kuzaliwa na sio lazima tujizoeshe kupumua vizuri. Je, ni kweli?

Kulingana na tafiti za hivi karibuni, inaonekana kwamba kuna mbinu fulani ya kujifunza.

Miongoni mwa mambo mengine kwa sababu si sawa kupumua kwa pua kama ilivyo kupumua kwa mdomo.Mtu hupumua kwa wastani kati ya lita 10,000 hadi 12,000 za hewa kwa siku.

Hewa haijalishi ni safi kiasi gani, ina chembechembe zilizositishwa kama vile vumbi, bakteria, virusi au vizalishaji vya kuvu ambavyo hutua kwenye njia ya hewa na sehemu za tundu la mapafu.Lakini tusiogope kabla ya wakati mfumo wa kupumua unajua jinsi ya kujisafisha na kujilinda.

Ukweli ni kwamba ni chembe chembe ndogo tu zinazoweza kufikia mapafu na kipenyo cha mikroni 3 hadi 5.Hupatikana kwa maelfu katika utando wa ukamasi katika njia ya kupumua kila seli ya utando wa pua na mishipa ya hewa ina silia 25 hadi 30 na urefu wa wastani wa mikroni 5 hadi 7.

Silia hujitokeza kwenye seli na kusonga kama fagio tunapofagia. Kazi yake ni kusafisha pua yaani chembe za kipenyo cha hadi milimita 0.5 zinazoingia zikiwavuta kuelekea kwenye koromeo ili ziondolewe kwenye pua kwa dakika 10 au 15 tu.

Nguvu kubwa ya mashujaa hawa wa seli ni kasi yao kuu wanatetemeka zaidi ya mara elfu moja kwa dakika wakisimamia kusukuma kamasi inayozunguka bomba kuelekea juu na kunasa vijidudu na chembe za vijidudu kwenye safu hii ya kamasi.

Mara baada ya hapo, mtu anaweza kuzikohoa au zikavutwa ndani ya kinywa ambapo hakuna silia, na kumezwa. Hiyo inawafanya kuwa utaratibu muhimu wa ulinzi dhidi ya maambukizo ya pua, matundu ya pua na mirija ya hewa.Pua imefunikwa na mshipa wa kipekee.

Katika kiwango cha kinga pia ni maalum kwa sababu ya vimelea vya magonjwa vinavyoingia na hewa tunayopumua.

Utando wa kamasi ndani ya pua unaendelea kuamua kati ya kushambulia kimelea au kuruhusu kiwe, kwa sababu uharibifu unaosababishwa na vita vinavyopigwana ndani yake itakuwa mbaya zaidi kwa mwili wetu.

Utaratibu huu unamaanisha kwamba kuna uvumilivu fulani kwa vimelea vya magonjwa ambavyo kwa kawaida havituletei madhara makubwa.

Sehemu ya jukumu hilo la "ulinzi" inatekelezwa na aina ya seli B ambayo hutoa kingamwili iitwayo IgA, tofauti kwa kiasi fulani na IgG inayosambaa katika damu na ambayo tumesikia zaidi wakati wa janga hili.

 

Kinywa kimsingi ni mlango wa chakula vigumu na vya majimaji.

Kazi yake ni kukabiliana na vimelea vinavyojaribu kuingia na chakula tunachokula. Kwa hiyo, kama vile tusivyokula chakula kupitia pua, hatupaswi kupumua kupitia kinywa pia.

Kwa kuongezea, hewa inayoingia kupitia pua hubakia joto na hufukuza vijidudu.Kupumua kwa mdomo hubadilisha mifupa ya uso

 

Kupumua kwa kawaida kwa kinywa kunaweza kusababishwa na sababu za kijeni, tabia za utumiaji mbaya wa mdomo au kuziba kwa pua, uwepo wa mianzi ya pua na kudhurika kwa utando wa pua.

Zaidi ya hayo, kupumua kupitia kinywa kunaweza kuhusishwa na mizio ya kupumua, hali ya hewa, au kulala vibaya.Na haipaswi kupuuzwa. Kupumua kwa mdomo kunaweza kubadilisha mpangilio wa mifupa ya uso kwa watoto.

Kwa mujibu wa mapitio ya kisayansi kulingana na uchambuzi wa meta, kupumua kwa njia ya kinywa husababisha mabadiliko katika ukuaji wa mifupa ya uso na mpangilio mbaya wa meno kwa watoto kunakoweza kusababisha mdomo kutofunga vizuri.Tatizo ni kwamba kufunga kinywa vibaya husababisha matatizo katika kiwango cha misuli ya kutafuna, shingo, na hata husababisha maumivu ya kichwa kwa watu wazima.

Zaidi ya nusu ya watoto wenye umri wa miaka 12 wanaugua ugonjwa wa meno kutokuwa katika sehemu yake kulingana na ripoti ya uchunguzi wa afya ya kinywa wa 2020 iliofanywa na Jarida la Baraza Kuu la Vyuo Vikuu vya Madaktari wa Meno Uhispania.

Kwa watu wazima, kinachostahili kufanyika ni kurekebisha mkao ikiwa tunapumua kupitia midomo yetu: tunainamisha shingo zetu mbele na kubadilisha msimamo wa vichwa na shingo ili kurekebisha pembe ya koromeo na kuwezesha kuingia kwa hewa kwenye midomo yetu.Ikiwa bado hujashawishika kuhusu faida za kupumua kupitia pua yako, jaribu kupumzika.

Utaona kwamba unapumua kupitia pua yako kwa kawaida, wakati utahitaji kujilazimisha kupumua kupitia kinywa chako.

Tumia mdomo wako kupumua "katika dharura tu."

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii