Madereva watakiwa kuacha tabia ya kupokea simu kwenye vyombo vya usafiri

Afisa Mnadhimu wa  kitengo cha usalama barabarani Makao Makuu ya Polisi Dar-es- Salaam- SACP Butusyo Akim Mwambelo amewataka waendesha  vyombo vya moto kuzingatia sheria wakati wanapoendesha vyombo vyao kwa kuacha kupokea simu na badala yake kusimamisha chombo chake ili kusikiliza simu hiyo jambo ambalo litasaidia kupunguza ajali barabarani.

Akizungumza na Madereva  wanaondesha vyombo vya moto wakiwemo Maafisa usafirishaji (Bodaboda), Bajaji na waendesha Bajaji za mizingo (Guta) huko katika Uwanja wa Polisi Mabatini, Wilaya ya Nyamagana, Mkoa wa Mwanza, amewaasa madereva hao kufanya biashara kwa upendo kwa kugawana abiria na sio kuzidisha abiria ili tu waweze kupata kipato "lazima kila mmoja wenu aweze kugawana kipato na wenziwe kwani hili linawezekana kukiwa na upendo"

 Vilevile Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi kutoka Makao Makuu ya kikosi cha Usalama barabarani ASP-Mwashamba Rashid Onesmo  amewaasa madereva hao kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani wakati wanaendesha chombo cha moto ili kuepusha ajali zisizotarajiwa.

Aidha amewasisitiza kusoma kwa ajili ya kupata leseni hai katika vyuo  vinavyotambulika kisheria, ili kuepuka udanganyifu pamoja na kukosa leseni inayotambulika kisheria.

Naye, mmoja wa madereva hao Abdallah Bakari amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kuja kutoa elimu hiyo kwani kuna baadhi ya madereva hawajui sheria za usalama barabarani, na kuhakikisha kuwa elimu hii  itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali za barabarani.

#10YrsJembefm  #Familiamoja #AhsantekwaTime

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii