Barack Obama na Michelle Obama Watoa Ufafanuzi kuhusu Kupeana Talaka

Hatimaye Rais Mstaafu wa Marekani Barack Obama na mke wake Michelle Obama, wametolea ufafanuzi kuhusu taarifa zinazosambaa kuwa ndoa yao ipo katika “mgogoro”.

Mapema mwanzao mwa mwaka huu, kulienea taarifa mbali mbali kuwa wawili hao hawana maelewano mazuri katika ndoa yao, hivyo wanashughulikia suala la talaka ili kila mmoja aendelee na maisha yake.

Wakitolea ufafanuzi kuhusu suala hilo katika mahojiano ya kipindi kinachorusha maudhui kwa njia ya mtandao (Podcast) kinachoitwa MO, mbacho huongozwa na Michelle Obama pamoja kaka yake, Craig Robinson, wanandoa hao wamesema ni kweli wanafahamu kuhusu uvumi huo, lakini hauna ukweli wowote.

Kwa Upande wake Michelle Obama amesema kuwa, ni kweli kuna changamoto na magumu ambayo yanajitokeza mara kadhaa kwa, lakini hilo haliwezi kumfanya aachane na mume wake

“Haijawahi kujitokeza hali yoyote katika ndoa yetu ambayo imenifanya nifikirie kumuacha mume wangu. Kuna muda tumekuwa tukikutana na magumu, lakini tumekuwa na mazuri mengi pia. Hiyo imenifanya kuwa mtu bora kwa sababu ya mwanaume ambaye amenioa” alisema Michelle.

Aidha Barack Obama aliongeza kuwa, watu wasipowaona pamoja katika matukio mbali mbali, basi huhisi kuwa wawili hao wanataka kuachana, kitu ambacho sio kweli.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii