Aidha, Theluji imeathiri usafiri katika majimbo ya kati na kusini mpaka mashariki mapema Jumatatu, na kupelekea shule na ofisi za serikali kufungwa katika majimbo kadhaa.
Barabara zote huko Kansas zilifunikwa, ikiwemo Nebraska magharibi na sehemu za Indiana, ambako Kikosi cha Ulinzi cha Taifa katika jimbo kilikuwa kikifanya kazi kuwasaidia wenye magari na takriban nchi 8 za theluji zilitarajiwa kuanguka, pamoja na upepo mkali wa kasi ya kilometa 72 kwa saa.
Zaidi ya watu milioni 60 katina nchi hiyo, wapo katika tahadhari ya hali ya hewa huku mtandao wa kufuatilia usafiri wa anga FlightAware ukionesha kufutwa kwa karibu safari 2,200 za ndege na nyingine zaidi ya 25,000 zikicheleweshwa.
Hali hatari sana ya hewa ya baridi ilitangazwa Januari 5, 2025 ikilikumba eneo kubwa la kati katikati mwa Marekani, huku dhoruba kali ikielekea upande wa mashariki, na kusababisha usumbufu kwa usafiri na kazi kutoka Kansas City hadi Washington DC.