Mpaka wa Kasumbalesa kati DRC na Zambia unafunguluwa tena Jumanne asubui Agosti 12, 2024, baada ya kufungwa kwa muda wa siku tatu. Kituo hiki cha mpakani ni cha pili kwa umuhimu nchini DRC baada ya Kinshasa. Uamuzi wa kufunguliwa upya ulichukuliwa jana Jumatatu mjini Lubumbashi kufuatia mkutano kati ya waziri wa Biashara wa Congo na mwenzake wa Zambia.