Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa kwa awamu ya pili ya uchaguzi wa urais

Wapiga kura milioni 60 wameitwa kupiga kura. Raia wa Iran watachagua kati ya mwanamageuzi Massoud Pezeshkian na Saïd Jalili ambaye ni mhafidhina mwenye msimamo mkali. Katika duru ya kwanza, kiwango cha ushiriki hakikufikia 40%, kiwango cha chini kabisa katika miaka 45. Kuzorota kwa hali ya kiuchumi inaelezea kwa kiasi kikubwa kususiwa kwa uchaguzi, kulingana na mamlaka.



Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii