KATAKISITA ABAKA MTOTO WA MIAKA 8

Jeshi la polisi mkoani Geita, linamshikilia Athanas Rugambwa (62) mkazi wa Muganza wilayani Chato mkoani Geita kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka nane mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Katema.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo Alhamis Septemba 15, 2022 Kamanda wa Polisi Geita, Henry Mwaibambe amesema mtuhumiwa ni katekista na alikua akimfundisha mtoto huyo masomo ya dini.

Ameeleza kuwa mtuhumiwa huyo alimvizia mtoto akiwa kwenye mafundisho ya dini kanisani na kumuita ofisini kwake kisha kumbaka.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii