Prince Dube Aomba Kuondoka Azam, Apewa Ruksa

Klabu ya Azam FC imethibitisha kupokea barua kutoka kwa mshambuliaji wao wa Kimataifa wa Zimbabwe, Prince Dube akiomba kuvunja mkataba na Klabu hiyo.

Ikumbukwe kuwa mkataba mpya wa nyota huyo raia hiyo aliyosaini mwaka 2023 ulipaswa kufikia ukingoni June 2026.

Azam FC imeweka bayana kuwa haina kipingamizi chochote na imemruhusu Dube kuondoka lakini matakwa ya kuvunja mkataba huo yafuatwe.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii