Kocha US Monastir atuma salam Young Africans

Kocha Mkuu wa US Monastir ya Tunisia Darko Novic amesema wapo tayari kuikabili Young Africans kwenye mchezo wa Mzunguuko wa Kwanza wa Kundi D, Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

US Monastir itaanzia nyumbani Stade Hammadi Agrebi, mjini Tunis, Februari 12 majira ya saa kumi na moja jioni kwa saa za Tunisia.

Kocha Novic amesema dhamira yao kuu ni kuhakikisha wanaanza vizuri michuano hiyo kwa kuifunga Young Africans, ambayo amekiri ina kikosi kizuri chenye uwezo wa kucheza popote Barani Afrika.

Amesema wanajiandaa kuelekea mchezo huo na wameifuatilia Young Africans kwa ukaribu na kubaini baadhi ya mbinu wanazotumia wanapokua nje na ndani ya Uwanja, hivyo itakua rahisi kwao kukabiliana nayo wakiwa nyumbani kwao Tunisia.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii