Azikwa akiwa hai huko Madaba.

Mzee Jonas Komba (78) Mkazi wa kijiji cha Mahanje Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma amezikwa akiwa hai na Wananchi wenye hasira kali kwa kushirikiana na baadhi ya Wanafamilia kutokana na tuhuma za kumuua Mtoto wake Severen Komba (34) aliyekutwa amefariki ndani ya nyumba yake.

Mkuu wa Wilaya ya Songea Pololeti Mgema amesema jambo hilo ni la kinyama kwa kuwa Wananchi wamejichukulia sheria mkononi kwa kumzika Mzee huyo akiwa hai badala ya mwili wa Mtoto huyo ambaye tayari alikutwa amefariki asubuhi bila ya kujulikana sababu za kifo chake, Mzee huyo amepoteza maisha baada ya kuzikwa akiwa hai.

Pata Habari Kupitia Mitandao Yetu Ya Kijamii